MASHINDANO YA DINDAI CUP YAZINDULIWA LEO KATIKA UWANJA WA PEPSI CHAMAGUHA.

Na

Paschazia Charles 

Uzinduzi wa mashindano ya Dindai  Cup  umefanyika leo June1, 2026 katika uwanja wa Pepsi uliopo kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga Mkoani Shinyanga.

Akizungumza katika hafla hiyo Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa mashindano hayo  Bi. Lilian Kashega ambaye ni Mkaguzi wa POLISI kata ya Chamaguha  amewataka Vijana  kuacha kujihusisha na tabia zisizo na faida ikiwemo  ulevi, uvutaji wa  madawaya kulevya.

Pia ameiasa jamii kuachana na vitendo vya ukatili kwa wengine wakiwemo watoto, Wananwake na jamii mzima.

Kwa upande wao Viongozi wa Chama Cha mpira Wilaya ya Shinyanga SHIDIFA wameishukuru Mfadhili wa mashindano  hayo na kwamba ameeandaa mashino hayo  lengo  kubwa ni kuinua vipaji vya Vijana wadogo  katika Manispaa ya Shinyanga.


Timu shiriki katika mashindano hayo ya Dindai Cup ni Chamaguha Fc, C-Coy Sc, Busulwa Sports Academy, Katunda Fc, Chipukizi Fc, Iwelyangula Fc, Home Boys Fc, Kabondo Fc  katika msimu huu wa  mashindano ya DINDAI  CUP  2026.

Katika mechi ya ufunguzi  siku ya leo  kati ya Chamaguha vs Kabondo Fc kutoka Galaba Kolandoto imemalizika kwa suruhu na mechi ya marudianao itafanyika siku ya ijumaa June 5,2026 katika uwanja wa Pepsi Kata ya Chamagua

Siku ya kesho mashindano yataendelea  kati ya  Iwelwangulya vs Home Boys katika uwanja wa Pepsi Kata ya Chamaguha Manispaa ya Shinyanga.















Download/Pakua/Install App ya APA HABARI Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia apahabarikadama@yahoo.com
Previous Post Next Post